-->

Kajala Masanja Ashangazwa na Kiki za Kutembea na Waume za Watu

STAA kiwango kunako filamu Bongo, Kajala Masanja kwa mara ya kwanza ameweka wazi kuwa hakuna kitu ambacho anakichukia katika maisha yake kama mtu kumbambikia kiki ambazo zinahusiana na kutembea na mume wa mtu au bwana wa mtu kwa sababu haimjengei chochote kwenye jamii zaidi ya kumuharibia.

Akizungumza na mwandishi, Kajala, alisema kuna watu wengi wako radhi kutengeneza kiki kama hizo za kuchukuliana mabwana lakini kwake hazitaki na zinamkera sana kwa sababu mambo hayo yameshapita na wakati na kwanza pia hayamjengei chochote kwenye jamii zaidi ya kumuharibia.

“Kiki kama hizo sizitaki kabisa kuzisikia kwanza zinaniharibia wala hazinijengi chochote kwenye jamii yangu zaidi ya kuniletea picha tofauti kwenye jamii yangu,” Kajala alionya.

Kajala ametoa ushauri huo ikiwa kuna fukuto la Hamissa Mobetto kutangaza kwamba amezaa na Diamond ambaye ni baba wa watoto wawili kwa Zari Hassani.

 

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364