-->

Odama: Hakuna wa Kuniondolea Heshima Yangu

Odama

Odama

Staa wa Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amesema kuwa tangu alipoingia katika usanii kitu kikubwa alichokuwa akikilinda ni heshima yake na si kitu kingine hivyo anayejaribu kuishusha afanye kazi ya ziada.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Odama alisema kuwa tangu ameanza kuwa msanii alijitahidi sana kuilinda heshima yake ndiyo maana watu wengi wanapenda kumjua baba wa mtoto wake lakini imekuwa vigumu.

“Watu wengi wanapenda kuishusha heshima yangu lakini nawaambia wajipange sana kwa sababu mimi ni mwanamke ninayejitambua hivyo kuishusha ni kazi ngumu sana mpaka hapa nilipofika,” alisema. Odama.

Chanzo: GPL

Comments

comments

Post Tagged with

Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364