-->

Rose Ndauka: Filamu Bongo Hazijashuka

Staa wa Bongo Movie, Rose Ndauka amedai kuwa ni upepo mchafu umepitia soko la filamu nchini na si kama ni kweli filamu zimeshuka thamani kama watu wanavyodai.

ROSE NDAUKA345

Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa baadhi ya wasanii wanazidi kujitahidi kufanya vizuri lakini kilichopo kwa sasa ni upepo mchafu umepitia tu.

“Huu ni upepo mchafu umepita lakini wasanii wanajitahidi sana kufanya filamu nzuri. Tumeweza kuona wakina Wema Sepetu wameenda mpaka Ghana kufanya movie na wasanii wa nje. Soko la filamu halijashuka kwa kuwa bado mashabiki wanaendelea kufuatilia na kusupport,” amesema Ndauka.

Rose ameongeza mashabiki watarajie filamu nyingine mwakani kutoka kwa wasanii wa ‘Ndauka Family’ kwa sasa waendelee kufurahia filamu ya ‘Angela’ iliyotoka mwezi Mei, mwaka huu.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364