-->

Bongo Movie ni Muda Wetu wa Kurelax – Aunt Ezekiel

Muingiza Aunt Ezekiel amesema Bongo Movie haijafa ila ni muda wao wa kupumzika ili kujipanga.

Aunt Ezekiel

Mrembo huyo amefafanua kuwa hiki ni kipindi cha wao kujipanga na wale wanaofikiri Bongo Movie haitarejea katika kiwango chake wanakosea.

“Bongo Movie tunaweza kusema ni kama maisha ya binadamu, kuna time analala, anaamka, anapika, so kunakuwa na kazi tofauti tofauti. Naweza kusema kwa sasa hivi Bongo Movie ni muda wetu wa kurelax kwanza kwa hiyo tumepumzika, tumelala tukishaamka nadhani tutakuja na vitu vingi vya tofauti,” Aunt Ezekiel amekiambia kipindi cha Twenzetu cha Times FM.

“Sio kwamba tukilala ndio hakuna kitu ambacho kitakuja kikubwa zaidi au hakitachukua akili za Watanzania tena, hapana kulala kwa Bongo Movie ni kulala kwa kujipanga ili tunapokuja kurudi tena turudi vizuri, so mimi siamini kama Bongo Movie imekufa, tumerelax tu,” ameongeza.

Bongo5

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364