Artists News in Tanzania

Nimekamua Kichizi Filamu ya Kitonga – Mau Fundi

MAULID ALLY aka Mau Fundi ametamba kwa kusema kuwa amefanya makubwa katika filamu inayokwenda kwa jina la Kitonga ambayo ameigiza kama mtu asiyependa masihara na anaamini kuwa ameitendea haki na wapenzi wa filamu wanunue waone kazi yake humo ndani.

“Nimekamua kichiz katika filamu ya Kitonga si unajua nikiwa na njaa ya kazi ninavyopiga kazi, leo jumatatu usikose kununua filamu ya Kitonga uone balaa langu humo nimetambaa kinoma si mchezo,”anatamba Mau.

Naye mtayarishaji wa filamu hiyo Juma Mtetwa ‘J Silk’ amesema kuwa sinema hiyo imeingia leo sokoni ikiwa na mastaa kibao waliofanya vinzuri katika tasnia kama Dennis David ‘D Touch’, Jackson Kabirigi, Mau Fundi, Taiya na wasanii wengine wakali katika tasnia ya filamu.

Filamu Central

Comments

comments

Exit mobile version