Artists News in Tanzania

Picha: Diamond na Mafikizolo Wakiwa Bungeni Leo

Kundi maarufu la muziki kutoka Afrika Kusini Mafikizolo pamoja na staa wa bongofleva Diamond Platnumz leo walipata mwaliko wa kuingia Bungeni Dodoma ambapo mastaa hawa wapo Dodoma kwa ajili ya kupiga burudani  Chuo kikuu cha Dodoma.

“Unajua leo tuna show hapa Dodoma mimi na Mafikizolo hivyo serikali kupitia kwa Waziri Nape Nnauye walitualika bungeni japo ni kwa muda mchache lakini kitendo hiki kinaonyesha jinsi gani serikali yetu inajali wasanii, unajua hawa wenzetu wanapokuwa kwao na sisi tunapokwenda huwa tunapata mapokezi mazuri sana hivyo na mimi nashukuru kwa hili kwani itafanya hata wenzetu wajue serikali yetu inajali wasanii wake”. alisema Diamond Platnumz.

Comments

comments

Exit mobile version