Artists News in Tanzania

Pichaz: Wema Sepetu na Wenzake Waitikia Wito wa RC Makonda

Kufuatia agizo la mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuwataka baadhi ya mastaa wanaoshukiwa kujihusisha na matumizi na biashara ya madawa ya kulevya kuwasili kituo cha polisi cha kati siku ya leo baadhi ya mastaa wametii agizo hilo na kuwasili.

Wema Sepetu akiwa Central Polisi

Malkia huyo wa filamu ambaye alikuwa mmoja kati ya wasanii waliotuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Da es salaam Paul Makonda kwamba anatumia Madawa ya kulevya, amewasili kituoni hapa nchana huu  huku akiwa amevalia vazi hijab.

Wasanii wengine waliofika kituoni hapo ni pamoja na TID, Nyandu Tozzy pamoja na mtangazaji wa Clouds TV Babu wa Kitaa.

Nyandu Tozi

TID akiwa kituoni hapo

 

 

Comments

comments

Exit mobile version