Artists News in Tanzania

Sasa ni Ben Pol vs Ramadee

Hatimaye msanii Ben Pol ameamua kumaliza utata uliopo kwa mashabiki kwamba kati yake na Rama Dee nani bingwa wa minyoosho kwenye R&B kwa kuamua kufanya naye collabo.

Ben Pol ambaye ameachia album yake yenye kazi zake bora ‘The Best of Ben Pol’, amemvuta Rama Dee kwenye remix ya ‘Pete’, na kukuachia wewe msikilizaji uamue nani kaifanya vizuri zaidi.

Albam hiyo ya Ben Pol imebeba nyimbo 11 ambazo zilifanya poa, huku zingine akizifanyia remix, na zingine ambazo ni mpya ikiwemo ile aliyomshirikisha msanii Chidinma wa Nigeria.

Comments

comments

Exit mobile version