-->

Tunda Afungukia Mimba ya Mbongo Fleva

BAADA ya habari kuzagaa kwamba mrembo anayeuza nyago kwenye video mbalimbali Bongo, Tunda Sebastian kuwa na ujauzito wa staa wa Bongo Fleva, ameibuka na kufungukia ishu hiyo.


Akizungumza na Star Mix, Tunda alisema hana ujauzito wa msanii huyo kama watu wasemavyo na kwamba huwa
anamuweka katika mitandao ya kijamii husan Instagram kwa sababu ya kumsapoti katika kazi zake.

“Ndiyo kwanza nasikia kwenu, siyo kweli na sina mimba yake. Huwa namuweka Insta kumsapoti kikazi tu maana ni rafiki yangu sana lakini watu walivyoona hivyo wakaanza kuzusha maneno hayo kwamba ninatoka naye na nina mimba yake. “Kuhusu kunenepa, nimenenepa kwa sababu nimeridhika na maisha mazuri niliyo nayo,” alisema Tunda.

Chanzo:GPL

Comments

comments


Unataka kutangaza nasi? Tumia namba ya simu hapo chini.

Please contact us: email : info@bongomovies.com or Mobile: +255 756 348 364