Mkurugenzi wa Shule za Sekondari za Waja Mkoa wa Geita, Eng. Chacha Wambura amewazawadia magari wanafunzi wake waliohitumu Kidato cha Sita katika Shule za Sekondari Waja Girls
baada ya kufanya vizuri katika masomo yao.
Kutoka kwenye tovuti ya shule, zawadi imekuja baada ya wanafunzi hao kuwa katika “TOP 10” ya wanafunzi waliofanya vizuri katika kidato cha Sita kwa mwaka 2017.
Wanafunzi hao ni Edna Meela na Byera Kaibagarauka ambao kila mmoja amezawadiwa gari lenye thamani ya fedha za kitanzania shs. 11,500,000.
Pia uongozi wa shule waliposoma itawapatia petrol lita 40 kwa kila mwanafunzi kwa kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja. Pia shule inawapa ofa nyingine ya kujifunza udereva ili wawezi kuyatumia magari yao.
Comments
comments