WASTARA Juma ambaye alikataa mahari ya shilingi milioni tano ya kijana Juma Mbega ‘Masairo’, hivi karibuni walionekana laivu katika picha za pozi tofauti walizopiga sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Inadaiwa kuwa wawili hao awali walikuwa wakiishi nyumba moja, enzi za uhai wa marehemu mume wa Wastara, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ ambaye alikuwa ni rafiki yake, hivyo kijana huyo kuwa kama shemeji wa muigizaji huyo.
Inadaiwa katika ukaribu wao wa sasa, wawili hao wamekuwa wakikesha studio, ambako Juma anarekodi singo yake ya muziki.
Gazeti hili lilimtafuta Wastara, ambaye alikiri kuwa karibu na kijana huyo, lakini akidai anafanya hivyo kwa vile ni kama shemeji yake ambaye ameishi naye kwa muda mrefu.
Kwa upande wake, Juma alisema Wastara ni mtu anayemsaidia katika mambo mengi, lakini pia amemsogeza karibu ili kumfanya awe na furaha na kutowapa watu nafasi ya kumchezea.
“Sitaki kupinga kuwa Wastara ni mtu muhimu sana kwangu, na sitaki kumpa nafasi mtu yeyote yule kumuumiza na kumkosesha furaha kwa sababu najua aliyekuwa akimpatia ni kaka yangu tu Sajuki,” alisema Juma.
Chanzo:GPL
Comments
comments